Mimi naitwa Michael T. Mwakilasa, ni mzaliwa wa Kyela, Mbeya. Nimesoma shule za msingi za Kyela, Mwadui na Mgulani kabla ya kwenda Tambaza, Mazengo na CBE.
Hivi sasa naishi Jersey City, NJ na mke wangu Prisca. Mwenyezi Mungu katubariki watoto wawili wa kiume Abraham na Baraka.
Familia yangu na matukio mbalimbali katika picha.
_________________________________________________________________
Tangu nikiwa mdogo nimekuwa nafanya biashara ndogo ndogo wakati huo huo nasoma, kwa muda sasa nimekuwa najifunza hii teknolojia ya intaneti na nadhani itakuwa njia mojawapo kubwa itakayotuletea watanzania maendeleo kwa upesi zaidi.
Hii tovuti nimeianzisha ili niweze kupata habari, huduma na burudani za Tanzania sehemu moja, kwani kuna habari kwenye tovuti na blog mbalimbali za watanzania ambazo kila siku napenda kuzipitia, nategemea utapenda mkusanyiko nilioufanya. Hivi karibuni nimeanza kutengeneza tovuti nyingine Best-Tanzania-Travel-Guide.com
Baadaye nikaanza kuwaonyesha hii tovuti marafiki zangu wakaniomba niipanue zaidi na niweze kuwakaribisha na watanzania wengine watakao pendezeshwa na mkusanyiko uliomo kwenye hii tovuti.
Kama utapenda kuanzisha tovuti, na umeupenda mfumo wangu tafadhali ingia hapa chini
________________________________________________________________
Tafadhali usisahau kijiandikisha kupata Gazeti Pepe la kila mwezi kwa kubonyeza kidude kinachosema RSS cha rangi ya machungwa pembeni kushoto kwani utakuwa unajulishwa pishi nyongeza yeyote inapotokea kwenye tovuti ya mtukwao.
Jiandikishe hapa chini, Ninaahidi sitagawa wala kuuza barua pepe yako bali nitaitumia kukuletea Gazeti Pepe la MtuKwao kila mwezi.