"Tazama ramani utaona nchi nzuri, yenye mito na mabonde mengi ya nafakaaa..."
Huwa nakaa nakumbuka nilipokuwa mdogo jinsi tulivyokuwa tunaimba huu wimbo!
Tanzania inasifika sana ulimwenguni kote kwa jinsi nchi yetu ilivyo maarufu kwa mbuga zetu, mlima Kilimanjaro, mito na maziwa yenye ndege adimu dunuani, visiwa vya Zanzibar na Pemba, amani, utulivu na upole wa watanzania.
Hebu tafadhali angalia hii video:
Kama wahenga walivosema "kwenye miti hakuna wazenzi". Mimi sijawahi kwenda kwenye mbuga za wanyama, sanasana nimeona wanyama mikumi wakati nasafiri kwa basi au reli ya Tazara kwenda Kyela kuona jamaa.
Mimi naamini watanzania wengi wanaoishi Tanzania na walioko nje hawajawahi kwenda kwenye mbuga za wanyama, wengine hawaoni umuhimu wake, wengine kipato ni kidogo, wengine wangepata habari za kutosha kuhusu jinsi ya kwenda pengine wangezitembelea!wengine wanasababu mbalimbali zingine.
Kama utapenda kutembelea mbuga zetu na ungependa ufahamu gharama na vibali zake, tafadhali ingia kwenye ukurasa wa regulations and park fees kwenye hii tovuti ya Hifadhi ya Taifa;