Mimi naamini, naweza nikawa nakosea! umuhimu wa kuwa na kibanda chako ni mkubwa sana nyumbani kuliko nchi za nje watanzania wengi wanakoishi. Kwanza ni urithi kwa familia yako, heshima na ni kwako hapo baadaye utakapokuwa mzee patakuifadhi.
Watanzania wengi wanaioshi nje wanaweza kununua nyumba kwa mfumo wa kukopeshwa, mradi tu wana kazi na ulipaji wao wa madeni si mbaya sana!
Katika kuhangaika kutafuta viwanja au kujenga, watanzania waishio nje wana habari nyingi tofauti, nyingine za kufurahia, kuchekesha na nyingine za kusikitisha.
Kuna kampuni nyingi zinazosaidia shughuli mbalimbali za makazi nyumbani kama unampango wa kutaka kununua nyumba au kupanga, au unafuta kiwanja;
Tanzania tujitahidi tuanze kufanya mambo kama ya hawa wenzetu wa Ghana.
Tovuti mbalimbali zinazohusu shughuli za makazi nyumbani;