Home
Blog ya MtuKwao
Tovuti Zetu
Huduma
Burudani
Matukio
Biashara
TV Live
Kujitolea
Makazi
Gazeti la Mwezi
Washauri
Tanzania
Kuhusu Mimi
Tuwasiliane

XML RSS
What is this?
Add to My Yahoo!
Add to My MSN
Add to Google
 

Biashara na Maendeleo

Kutokana na takwimu za vyama vya kimataifa, uchumi wa bara la afrika unakua kwa kasi zaidi kuliko mabara mengine.

Tanzania ni nchi mojawapo iliyojuu katika takwimu hizo. je, hali hiyo itatusaidiaje watanzania kuweza kuanzisha biashara na kuongeza ajira kwa watanzania wengi?

Ukiwa na mipango ya kufanya au bado unafanya utafiti wa biashara gani unataka kuifanya nyumbani, tafadhali unaweza kutumia tovuti zifuatazo kukusaidia zaidi;

------------------------------------------------------------

-Business Registrations and Licensing Agency(Brela)

-Orodha ya Mabenki mbalimbali

-Tanzania Chambers of Commerce

-Tanzania Development Gateway

-Tanzania Investment Centre(TIC)

-Dar Stock Exchange(DSE)

------------------------------------------------------------

Kuna mikutano mbalimbali ya wafanya biashara wa kutoka nje inayofanyika Tanzania kila mara. Mkutano mmoja wapo maarufu utakaowaleta wafanyabiashara Wamarekani weusi utafanyika Arusha mwezi wa 6 kuanzia tarehe 2 mpaka 6, kwa taarifa zaidi bofya hapa


Je, Afrika tuko tayari kwa biashara!


Nimefurahishwa sana na hawa ndugu zetu wa nchi za kiafrika walioamua kutumia ubunifu, ujuzi na bidii bila kukata tamaa ya hali waliyokuwa nayo katika nchi zao na kuanzisha biashara zilizofanikiwa. Mimi naamini watanzania tunaweza kujifunza kitu fulani kutoka kwao.

Hebu mwangalia huyu mama wa kinigeria - Mama Adenike Ogunlesi alivyoanzisha nguo za watoto anazoziita Ruff 'N' Tumble.

________________________________________________________________

Benki ya HFC Ghana Ltd wanavyowasaidia waghana kununua nyumba kwa kuwakopesha mikopo.

________________________________________________________________

Hargeisa, Somalia - Bwana Mohammed Olad alianziasha shirika la ndege wakati hakuna hata serikali!

_______________________________________________________________

Kinshasa, D.R. Congo - Bwana Alieu Conteh alianzisha uwakala na Vodacom bila kujali hali mbaya ya vita Kongo!

________________________________________________________________

Kampala, Uganda - Bwana Michael Kiijambu ameanzisha maduka ya kuuza kahawa inayoitwa "1000 Cups Coffee House"

________________________________________________________________

Livingstone, Zambia - Bwana Ndaba Ndlovu alianza kama guide sasa hivi anaendesha kampuni yake ya "Touch Adventure" kwa watalii wanaopenda starehe za kukufanya damu iende mbio!

_______________________________________________________________

Huyu Bi Monique Maddy alikuwa na kampuni Tanzania ya simu iliyokuwa inaitwa Adesemi katika miaka ya mwishoni mwa tisini na mwanzoni mwa elfu mbili, ameandika kitabu na anaelezea kidogo kuhusu kitabu chake;

Msikilize Bwana Ali Mufuruki Mkurugenzi mkuu wa InfoTech akituwakilisha kwenye kongamano moja la kimataifa kuhusu jinsi gani ya kusaidia biashara za nchi za dunia ya tatu hasa hasa kuhusiana na fedha iliyoandaliwa na Google

Nadhani hili ni somo zuri sana kutoka kwa hawa wote wanne.


footer for Biashara page